Ndugu mteja,
Ni furaha yangu kupata fursa hii kuwasilisha kwako Mkataba wa Huduma ya Mteja. Huu ni Mkataba ambao unalenga katika kutoa huduma ambayo tumejipanga kukuhudumia kama Mteja wetu. Mkataba huu umeainisha viwango vya huduma, haki na wajibu wako ambavyo kwa pamoja vinatuwezesha kutimiza matarajio yako.
Tunawajibika kukupatia huduma sahihi na rahisi ambayo haina ubaguzi ili kujenga mahusiano yenye kuaminiana na kuheshimiana. Tunakutambua kama mteja mshirika wetu muhimu katika masuala ya usimamizi wa kodi.
Ninasisitiza tena ahadi ya TRA katika kuhakikisha matarajio yako yanatimizwa leo na wakati wote. Tunakuhimiza "TIMIZA WAJIBU TUKUHUDUMIE IPASAVYO" ili kufikia malengo tuliyojiwekea.
KAMISHNA MKUU
Habari & Matukio
WAZIRI WA FEDHA AKABIDHI TUZO ZA MAWAZO YA UBUNIFU ZA TRA
BANDARI KAVU SASA KUFANYA KAZI SAA 24
CG MWENDA AZINDUA BODI YA TRA UNITED
TRA YAFUNGUA KITUO KIPYA CHA HUDUMA ZA KODI MASAKI DSM